WATANZANIA WATAKIWA KUSHIKAMANA NA KUIPENDA NCHI YAO
Na. Jovina Bujulu – Maelezo
WATANZANIA wametakiwa kushikamana, kupendana na kulinda rasilimali zao kwani wao ndio wenye mamlaka ya kuendesha nchi yao.
Wito
 huo umetolewa leo jijini Dar es slaam na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar
 es Salaam, Idara ya Sayansi na Siasa Dkt. Bashiru Ally  wakati
 wa mahojiano na Mwandishi wa habari kuhusu mafanikio ya miaka 55 ya 
uhuru wa Tanzania ambayo yatafikia kilele tarehe 9 Desemba.
Akizungumzia
 mafanikio ambayo nchi imefikia tangu ilipopata uhuru mwaka 1961 alisema
 kuwa Tanzania imefanikiwa kujenga umoja wa kitaifa hasa kwa kutumia 
lugha ya Kiswahili katika shughuli mbalimbali za Kitaifa na kimataifa.
“Matumizi
 ya Kiswahili katika kazi za kitaaluma, kibiashara na nyanja za sayansi 
yameimarisha umoja wa kitaifa” alisema Dkt. Bashiru.
Aidha
 Dkt. Bashiru alimpongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutumia 
lugha ya Kiswahili katika shughuli mbalimbali za kitaifa na kimataifa 
kwa kuwa lugha hiyo ina utajiri wa maneno hivyo ikutumika vizuri 
Tanzania itapiga hatua zaidi na kuimarisha mshikamano wa kitaifa.
Akizungumzia
 suala la nchi kuelekea uchumi wa viwanda vidogo na viwanda vya kati 
Dkt. Bashiru alisema kuwa ni vizuri viwanda vinavyoanzishwa  sehemu
 kubwa ya malighafi vikatumia rasilimali za nchini na vizingatie maslahi
 ya watanzania kwa misingi ya usawa, haki na utu ili vizalishe ajira kwa
 vijana wa Tanzania.
“Rais
 awaamini Watanzania ndiyo wazalishaji namba moja hasa wazalishaji 
wadogo na nguvu zielekezwe katika uzalishaji ili fedha zinazopatikana 
zielekezwe katika huduma za kijamii kama vile elimu, afya na maji”, 
aliongeza Dkt. Bashiru.
Kwa
 upande wa suala la nidhamu ,Dkt. Bashiru alisema kuwa kumekuwepo na 
mabadiliko makubwa kwa watumishi wa Umma ambapo wafanyakazi wanahi 
kazini, kutumia lugha nzuri na kupunguza vitendo vya kudai rushwa.
Alimpongeza
 Rais Dkt. Magufuli kwa juhudi anazozifanya za kukusanya mapato na 
kusimamia nidhamu ya matumizi ya fedha hizo na alimtaka asilegeze kamba 
katika kusimamia eneo la uzalishaji.
Alisema
 kuwa jitihada hizo ndio zimesaidia Shule kifurika wanafunzi kutokana na
 elimu bure, ongezeko la madawati mashuleni na mafanikio katika sekta ya
 afya na kilimo.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni