Jumatano, 30 Novemba 2016

KIGOMA MJINI WAMPONGEZA LUKUVI KUTATUA MIGOGORO YAO YA ARDHI


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi anaendelea na ziara ya siku tatu katika mkoa wa Kigoma ambapo amefungua rasmi Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoa wa Kigoma pamoja na kutatua migogoro ya ardhi ya wananchi wa Kigoma. Wananchi hao wamempongeza Mhe. Waziri kwa hatua anazozichukua katika kumaliza migogoro yao ya ardhi na kuwajengea Baraza la Ardhi na Nyumba ambalo jipya na lililo na viwango kushinda mengine yote hapa nchini.zit1
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi akifungua Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoani Kigoma, Kushoto ni Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Zitto Kabwe na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe.Brigedia Jenerali Emanuel Maganga.
zit2
Jingo jipya la Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoani Kigoma.
zit3
Samani mpya za Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoani Kigoma.
zit4
  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi akiongea na wananchi wa Kigoma Mjini na kutatua migogoro yao ya ardhi.
zit6 zit7
Wananchi wa Kigoma Mjini wakiwasilisha malalamiko yao ya migogoro ya ardhi kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi ili yaweze kutatuliwa.
zit9
Wananchi wa Kigoma mjini wakimsikiliza Waziri wa Ardhi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni