KIGOMA MJINI WAMPONGEZA LUKUVI KUTATUA MIGOGORO YAO YA ARDHI
Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi anaendelea na ziara ya siku tatu
katika mkoa wa Kigoma ambapo amefungua rasmi Baraza la Ardhi na Nyumba
la Mkoa wa Kigoma pamoja na kutatua migogoro ya ardhi ya wananchi wa
Kigoma. Wananchi hao wamempongeza Mhe. Waziri kwa hatua anazozichukua
katika kumaliza migogoro yao ya ardhi na kuwajengea Baraza la Ardhi na
Nyumba ambalo jipya na lililo na viwango kushinda mengine yote hapa
nchini.![zit1](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_tUPBD7-EoPFnmounDd0ukOWtcD5myf5-xqYc4yJHEMHNQn_B0MU2igZnGr5WbEXlOKqtVZvGso6_orqFeWxYrLMK8e6_2-acppbjYVS36WhWwhNVTaj7K8axgPqWOpVuqktZIDWw=s0-d)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi akifungua Baraza la Ardhi na
Nyumba la Mkoani Kigoma, Kushoto ni Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Zitto
Kabwe na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe.Brigedia Jenerali Emanuel
Maganga.
Jingo jipya la Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoani Kigoma.
Samani mpya za Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoani Kigoma.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi akiongea na wananchi wa Kigoma
Mjini na kutatua migogoro yao ya ardhi.
Wananchi wa Kigoma Mjini
wakiwasilisha malalamiko yao ya migogoro ya ardhi kwa Waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi ili yaweze kutatuliwa.
Wananchi wa Kigoma mjini wakimsikiliza Waziri wa Ardhi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni