SIMBA YASHUSHA KIPA MPYA TOKA MEDEAMA FC YA GHANA.
Baada ya
taarifa kuenea kuwa Simba inataka kusajili golikipa toka Ghana hatimaye
ametua rasmi kwa ajili ya kujiunga na kikosi cha Kocha Joseph Omog.
Kipa huyu Daniel Agyei alikuwa
anakitumikia kikosi cha Medeama FC ambayo ilicheza na Yanga katika
michuano ya Kombe la shirikisho barani Afrika.
Mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar, kipa huyo
alipokelewa na Mratibu wa Simba, Abbas Ally na atakuwa akitoa changamoto
kwa golikipa wa sasa Vicent Agban ambaye alikosa mshindani kutokana na
uwezo wa Manyika Peter na Denis Richard kuonekana kuwa hawakuwa na
kiwango cha juu pamoja na kukosa uzoefu katika mikikimiki.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni