STAR MEDIA (TANZANIA) LIMITED yazindua televisheni mpya  yenye king'amuzi ndani yake...
A ELIZABETH VICENT, Dar
KAMPUNI ya StarTimes Tanzania jana ilizindua televisheni 
mpya ya kidigitali ambayo ina king'amuzi ndani na itawezesha wateja wake
 kuangalia chaneli mbalimbali bila usumbufu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo,Mkurugenzi Mkuu wa Star 
Times Tanzania, Lanfang Liao alisema kuwa kama kampuni imeamua kutoa 
television hizo za kisasa kulingana na ukuaji wa teknlojia ambapo wateja
 wataweza kuona vipindi vinavyoendana na wakati.
"Tutahakikisha tunawapa wateja wetu vipindi vyenye ubora 
huku wakifurahia Ulimwengu wa kidigitali kwa bei nafuu, lakini tunafahu 
kuwa msimu huu ni wa sikukuu hivyo ni lazima wateja wapate kitu tofauti 
kitakachoafurahisha" alisema Liao
Akizungumzia ubora wa Televisheni hizo alisema kuwa ni 
miongoni mwa televisheni ambazo zimeunganishwa na king'amuzi moja kwa 
moja huku zikiwa na matumizi madogo ya umeme tofauti na televisheni za 
kawaida ambazo zenyewe hutumia WAT200 kwa saa.
Aidha Liao alisema kuwa televisheni hizo zina chaneli zaidi
 ya mia moja  ambapo zina uwezo wa kuonyesha vipindi mbalimbali vyenye 
kuelimisha na kuburudisha jamii.
"Televisheni hizo zina ukubwa tofauti ambapo zinapatikana 
kwa inchi 40,32, pamoja na inchi24 huku zikiwa na vifurushi vya mwezi 
mmoja bure" alisema.
Kwa upande wake Katibu Mkuu kutoka Wizara ya 
Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Maria Sasabo alisema kama serikali 
itaendelea kuchunguza kwa umakini bidhaa zinazotumia teknolojia ya 
kidigitali ili kupima uwezo wa bidhaa hizo nchini.
"Suala la Teknlolojia na mawasiliano linachukua nafasi 
kubwa katika taifa letu, hivyo kwa kitu chochote kinachozinduliwa ni 
lazima tupime ubora wake na hapa tunashukuru Star times kwa kutupatia 
serikali televisheni moja ambayo tutaenda kuipima kama wizara husika" 
alisema.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni