Ijumaa, 18 Novemba 2016

STAR MEDIA (TANZANIA) LIMITED yazindua televisheni mpya  yenye king'amuzi ndani yake...

A ELIZABETH VICENT, Dar

KAMPUNI ya StarTimes Tanzania jana ilizindua televisheni mpya ya kidigitali ambayo ina king'amuzi ndani na itawezesha wateja wake kuangalia chaneli mbalimbali bila usumbufu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo,Mkurugenzi Mkuu wa Star Times Tanzania, Lanfang Liao alisema kuwa kama kampuni imeamua kutoa television hizo za kisasa kulingana na ukuaji wa teknlojia ambapo wateja wataweza kuona vipindi vinavyoendana na wakati.

"Tutahakikisha tunawapa wateja wetu vipindi vyenye ubora huku wakifurahia Ulimwengu wa kidigitali kwa bei nafuu, lakini tunafahu kuwa msimu huu ni wa sikukuu hivyo ni lazima wateja wapate kitu tofauti kitakachoafurahisha" alisema Liao

Akizungumzia ubora wa Televisheni hizo alisema kuwa ni miongoni mwa televisheni ambazo zimeunganishwa na king'amuzi moja kwa moja huku zikiwa na matumizi madogo ya umeme tofauti na televisheni za kawaida ambazo zenyewe hutumia WAT200 kwa saa.

Aidha Liao alisema kuwa televisheni hizo zina chaneli zaidi ya mia moja  ambapo zina uwezo wa kuonyesha vipindi mbalimbali vyenye kuelimisha na kuburudisha jamii.

"Televisheni hizo zina ukubwa tofauti ambapo zinapatikana kwa inchi 40,32, pamoja na inchi24 huku zikiwa na vifurushi vya mwezi mmoja bure" alisema.

Kwa upande wake Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Maria Sasabo alisema kama serikali itaendelea kuchunguza kwa umakini bidhaa zinazotumia teknolojia ya kidigitali ili kupima uwezo wa bidhaa hizo nchini.

"Suala la Teknlolojia na mawasiliano linachukua nafasi kubwa katika taifa letu, hivyo kwa kitu chochote kinachozinduliwa ni lazima tupime ubora wake na hapa tunashukuru Star times kwa kutupatia serikali televisheni moja ambayo tutaenda kuipima kama wizara husika" alisema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni