PLAN INTERNATIONAL YAZINDUA MRADI WA KUWAWEZESHA VIJANA NA WATOTO KUPITIA MICHEZO.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa 
Wilaya ya Kisarawe, Mkoani Pwani, Wanchoko Chinchibera akiongea na 
wanafunzi pamoja na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Mradi wa 
Kuwawezesha Vijana na Watoto kwa Njia ya Michezo uliozinduliwa leo 
wilayani humo.Mradi huo unaratibiwa na Shirika la Plan International.
Meneja Miradi wa Shirika la Plan 
International, Grace Semwaiko akielezea kuhusu malengo ya mradi wa 
Kuwawezesha Vijana na Watoto kwa Njia ya Michezo uliozinduliwa leo 
wilayani Kisarawe.Mradi huo unaratibiwa na Shirika la Plan 
International.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa 
Wilaya ya Kisarawe, Mkoani Pwani, Wanchoko Chinchibera akikagua timu ya 
mpira ya watoto wakati wa mradi wa Kuwawezesha Vijana na Watoto kwa Njia
 ya Michezo uliozinduliwa leo wilayani humo.Mradi huo unaratibiwa na 
Shirika la Plan International.
…………………………………………………………………
  Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Shirika
 la Plan International limezindua Mradi wa Kuwawezesha Vijana na Watoto 
kwa Njia ya Michezo ili kuwajengea uwezo wa kuwa mawakala hai wa 
mabadiliko chanya katika jamii zinazowazunguka.
Mradi
 huo umezinduliwa leo Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani na Afisa Maendeleo 
ya Jamii wa Wilaya hiyo, Wanchoko Chinchibera ambaye ametoa wito kwa 
watendaji wa Serikali, wazazi pamoja na jamii kwa ujumla kutoa 
ushirikiano wa hali ya juu ili kuhakikisha mradi huo unatekelezeka.
Chinchibera
 amesema mradi huo umekuja wakati muafaka kwani watoto na vijana 
wanakabiliwa na changamoto ya ulinzi, usawa wa kijinsia pamoja na 
ushirikishwaji mdogo katika michezo hivyo kupitia mradi huo watapata 
maendeleo mazuri ya kielimu na kimakuzi pamoja na fursa ya kutatua 
changamoto zao.
“Kupitia
 michezo tunajenga afya, akili, malezi na makuzi ya mtoto lakini pia 
michezo ni sehemu ambayo watoto wanaweza kupaza sauti zao na kujadili 
kuhusu haki zao za msingi kwa njia ya nyimbo na mashairi hivyo tunaamini
 kuwa tukianza kuwashirikisha watoto katika suala zima la michezo 
tutatengeneza kizazi chenye maendeleo,”alisema Chinchibera.
Ameongeza
 kuwa kupitia michezo, vipaji vingi vitaibuliwa ambavyo vitasaidia 
katika kutengeneza ajira mbalimbali zitakazowawezesha vijana kujikomboa 
kiuchumi na kuchangia katika pato la taifa hivyo amewahakikishia 
wananchi kuwa mradi huo utazaa matunda mazuri.
Kwa
 upande wake Meneja Miradi wa Shirika hilo, Grace Semwaiko amesema mradi
 huo ni sehemu ya mpango mkakati wa tatu wa shirika hilo ambao kwa 
ujumla unalenga kufikia jumla ya watoto 3,075 na vijana 3,109 katika 
kuwahakikishia ulinzi na usawa wa kijinsia.
“Ni
 matumaini yetu kuwa mradi huu utatekelezwa vizuri na hatimaye kufikia 
malengo tuliyojipangia yakiwemo ya kukua kwa uelewa kwa jamii na wadau 
wote kuhusu usawa wa kijinsia, kuhakikisha vijana na watoto 
waliowezeshwa wanaleta mabadiliko katika jamii pamoja na kuimarika kwa 
ulinzi wa watoto katika ngazi ya jamii hadi taifa,” alisema Bi Grace.
Alifafanua
 kuwa mradi huo unawalenga wanafunzi wa Shule za Msingi kuanzia darasa 
la 4 hadi la 7, wanafunzi wa Shule 6 za Sekondari, walimu, wazazi, 
viongozi wa jamii na watendaji wa Vijiji, Kata pamoja na Watoto na 
Vijana ambao hawasomi.
Mradi
 huo utaratibiwa na shirika la Plan International pamoja na shirika la 
Right to Play na utatekelezwa katika Kata mbili za Kiluvya na Malumbo 
zilizopo wilayani humo ambapo jumla ya vijiji 10 vitanufaika.
Aidha
 Bi.Grace aliongeza kuwa Mradi huo unatarajiwa kuwa wa miaka miwili na 
utagharimu jumla ya shilingi 641,468,700 ambapo unatarajiwa kukamilika 
mwezi Juni 2018.
Shirika
 la Plan International la nchini Ujerumani ni miongoni mwa mashirika ya 
Kimataifa yasiyo ya kiserikali ambayo yameonyesha juhudi kubwa za kuibua
 miradi mbali mbali katika jamii na kuifadhili katika sekta za 
Afya,Maendeleo ya jamii,Wanawake,Watoto na Michezo.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni