Ijumaa, 20 Februari 2015

Wafunga ndoa wakiwa wamelala kwenye majeneza

Ilikuwa kama filamu au mchezo wa kuigiza, lakini kilichotokea kilikuwa kweli mbele ya macho ya watu. Ndoa 10 zilifungwa mwishoni mwa wiki iliyopita na kilichoshangaza zaidi ni wanandoa hao kufunga ndoa wakiwa kwenye majeneza katika mji wa Wat Takien, Jimbo la Nonthaburi nchini  Bangkok.
Wandoa hao walifikia uamuzi huo kutokana na imani kuwa kwa kulala kwenye jeneza muda mfupi baada ya kufunga ndo, kungeondoa mikosi kwenye maisha na kuwafanya kuishi maisha ya furaha.
Wanandoa hao walipanga majeneza yao yakiwa na rangi ya pinki na wakiwa ndani yake walilala pamoja kama vile maiti inavyohifadhiwa tayari kwa kuzikwa.
Majeneza hayo yalitengenezwa maalumu kwa ajili ya kuweza kulala watu wawili bila shida.
Kadhalika, wakiwa ndani ya majeneza, kila mmoja alishika ua na kulikumbatia kifuani, kabla viongozi wa kimila kufunika jeneza hilo kwa kutumia kitambaa cheupe ikiwa ni ishara ya kuondoa mikosi.
Kwa mujibu wa gazeti la Bangkok Post, wanandoa hao baada ya kutoka kwenye majeneza hayo, huanza maisha mapya wakiwa hawana mikosi kwa vile tayari inakuwa imeondolewa kwenye baada ya kumalziika ibada.
Hata hivyo, tukio hilo siyo mara ya kwanza kutokea nchini humo, kwani mwaka jana wakati wa shehere za siku ya wapendanao zilifanyika na kisha kufuatia na sherehe za kimila kama ilivyokuwa mwaka huu.
Lilipofanyika tukio kama hilo mwaka jana, hakukuwa na mapngo wa kulifanya tena katika mji wa Makha Bucha, lakini kutokana na maombi mengi kutoka kwa watu, ililazimu ukufanyika tena.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni