Ilikuwa
 kama filamu au mchezo wa kuigiza, lakini kilichotokea kilikuwa kweli 
mbele ya macho ya watu. Ndoa 10 zilifungwa mwishoni mwa wiki iliyopita 
na kilichoshangaza zaidi ni wanandoa hao kufunga ndoa wakiwa kwenye 
majeneza katika mji wa Wat Takien, Jimbo la Nonthaburi nchini  Bangkok. 
Wandoa
 hao walifikia uamuzi huo kutokana na imani kuwa kwa kulala kwenye 
jeneza muda mfupi baada ya kufunga ndo, kungeondoa mikosi kwenye maisha 
na kuwafanya kuishi maisha ya furaha.
Wanandoa
 hao walipanga majeneza yao yakiwa na rangi ya pinki na wakiwa ndani 
yake walilala pamoja kama vile maiti inavyohifadhiwa tayari kwa kuzikwa.
Majeneza hayo yalitengenezwa maalumu kwa ajili ya kuweza kulala watu wawili bila shida.
Kadhalika,
 wakiwa ndani ya majeneza, kila mmoja alishika ua na kulikumbatia 
kifuani, kabla viongozi wa kimila kufunika jeneza hilo kwa kutumia 
kitambaa cheupe ikiwa ni ishara ya kuondoa mikosi.
Kwa
 mujibu wa gazeti la Bangkok Post, wanandoa hao baada ya kutoka kwenye 
majeneza hayo, huanza maisha mapya wakiwa hawana mikosi kwa vile tayari 
inakuwa imeondolewa kwenye baada ya kumalziika ibada.
Hata
 hivyo, tukio hilo siyo mara ya kwanza kutokea nchini humo, kwani mwaka 
jana wakati wa shehere za siku ya wapendanao zilifanyika na kisha 
kufuatia na sherehe za kimila kama ilivyokuwa mwaka huu.
Lilipofanyika
 tukio kama hilo mwaka jana, hakukuwa na mapngo wa kulifanya tena katika
 mji wa Makha Bucha, lakini kutokana na maombi mengi kutoka kwa watu, 
ililazimu ukufanyika tena.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni