Kamati maalumu ya Shirikisho la Soka Ulimwenguni (Fifa), imesema kuwa kama fainali hizo zitachezwa katikakati ya mwaka kama ratiba inavyotaka, zinaweza kuwaathiri wachezaji na mashabiki ambao hawajazoea hali hiyo ya joto.
Hivyo basi, njia ya kunusuru hali hiyo ni kuipeleka mashindano hayo hadi Desemba ambako kunakuwa na nyuzi joto 25.
Mapendezo hayo yanatarajia kujadiliwa na Kamati ya Utendaji ya Fifa itakayokuna mjini Zurich, Uswisi kati ya Machi 19 na 20 March.
Kamati hiyo ya kufuatilia maandalizi inaongozwa na Sheikh Salman bin Ebrahim Al-Khalifa, ambaye pia amependekeza michuano hiyo kuchezwa kwa muda mfupi zaidi kuliko wakati mwingine wowote katika miaka ya hivi karibuni zilipoanza kushiriki timu zaidi ya 30.
Bosi huyo wa kamati amependekeza michuano hiyo kuanza Novemba 26 hadi Desemba 23, mwaka 2022
Hata hivyo, Fifa imesema haina mpango wa kupunguza timu kutoka 32 za sasa zinazocheza mechi 64
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni