WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROFESA SOSPETER MUHONGO AKUTANA NA WASAMBAZAJI WA GESI MAJUMBANI JIJINI DAR ES SALAAM
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akiongoza kikao kilichoshirikisha kampuni zinazohusika na usambazaji wa gesi majumbani pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC),  Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (PURA) na  Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa pamoja  nchini (PBPA).
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe (kushoto) pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC),  Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (PURA) na  Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa pamoja  nchini (PBPA), wakifuatilia maelekezo  yaliyokuwa  yanatolewa na Waziri wa Nishati na Madini  Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani)
Watendaji kutoka kampuni zinazohusika na usambazaji wa  gesi majumbani  wakifuatilia maelekezo  yaliyokuwa  yanatolewa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani).
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisisitiza jambo katika kikao hicho.
Mkurugenzi Mtendaji kutoka Tanzania Association of Oil Marketing, Salum Busarara akieleza jambo katika kikao hicho
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni