SERIKALI MKOANI PWANI YAONGEZA MIEZI MITATU KUWABOMOLEA WALIO NDANI YA HIFADHI YA BARABARA NDANI YA MITA 60
 Mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo akizungumza na baadhi ya wafanyabiashara  na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Bwawani Kibaha.
Mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist 
Ndikilo akiingia kwenye uwanja wa Bwawani Mailmoja Kibaha kuzungumza na 
wananchi kuhusiana na zoezi la bomoa bomoa lililosogezwa mbele hadi 
January 23 mwakani.
Baadhi ya wananchi Mail moja Kibaha wakionekana kusikiliza mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo. 
(Picha zote na Mwamvua Mwinyi)
(Picha zote na Mwamvua Mwinyi)
………………………………………………………………………………………………….
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
SERIKALI mkoani Pwani ,imewaongezea 
muda wafanyabiashara na wananchi waliojenga kwenye eneo la hifadhi ya 
barabara kuu ya Dar es salaam –Morogoro waliotakiwa kubomolewa novemba 
23 mwaka huu badala yake itakuwa January  2017.
Zoezi 
hilo lilikuwa likihusisha walioingia ndani ya barabara hiyo kuanzia eneo
 la Kiluvya-Tamco na soko la Mailmoja ambapo wameongezewa miezi mitatu 
kutokana na soko jipya kuchelewa kujengwa chini ya halmashauri ya Kibaha
 Mji.
Mkuu wa
 mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo,aliyasema hayo wakati alipokuwa
 akizungumza na baadhi ya wafanyabiashara hao na wananchi kwenye mkutano
 wa hadhara uliofanyika viwanja vya Bwawani Kibaha.
Aliwataka wahusika hao kuanza kubomoa na kuhama kwa hiari ,ndani ya kipindi hicho kilichoongezwa kabla ya january 23 mwakani .
Hata 
hivyo mhandisi Ndikilo,alieleza kuwa wafanyabiashara hao hawataondolewa 
hadi halmashauri ya Mji wa Kibaha itakapojenga soko jingine.
“Maandalizi ya kuhamia kwenye soko 
jipya hayajakamilika na hakuna chochote kilichojengwa ambapo ni miezi 
miwili imepita toka TANROADS walipotoa notisi kwa waliojenga kwenye 
hifadhi hiyo kuondoka likiwemo na soko hilo”
“Maelekezo yametolewa na waziri wa 
ujenzi ,uchukuzi na mawasiliano kwamba zoezi la bomoabomoa ni mita 60 na
 siyo mita 120 kama ilivyoonyesha na kutangazwa na wakala wa barabara 
Tanzania (TANROADS)mkoa wa Pwani,”alisema mhandisi Ndikilo.
Mhandisi
 Ndikilo alisema  mkurugenzi Jeniffer Omolo kasema mkandarasi kapatikana
 hivyo namtaka ajenge soko ndani ya siku 30 ili ibakie kujenga vizimba 
na ujenzi uanze kuanzia wiki ijayo ili wafanyabiashara wapate eneo lao 
la kufanyia biashara zao.
Alisema
 ujenzi wa soko utafanyika kwenye eneo la Mnarani maarufu kama 
Sagulasagula ama Loliondo na wanatarajia kutakuwa na huduma muhimu 
ikiwemo maji na huduma nyingine zitapatikana.
Alifafanua
 muda uliopangwa wa miezi mitatu sawa na siku 90 vitu vyote viwe 
vimekamilika kwani hakutoongezwa muda mwingine hivyo wale waliojenga 
kwenye eneo ambalo ni hifadhi ya barabara ndani ya mita 60 waanze 
kuvunja wenyewe bila kusubiri kushurutishwa.
Mhandisi
 Ndikilo anasema  walionunua kwenye eneo la kitovu cha Mji wanapaswa 
kujenga haraka.Huu ni wakati wa jamii kukubali mabadiliko hayo ambayo 
yapo ndani ya sheria ili mji wa Kibaha uweze kuwa katika mpangilio 
mzuri.
“Lengo letu ni halmashauri ya Mji 
kuwa manispaa hivyo moja ya vigezo ni kupanga Mji huu ,wananchi 
watuelewe na wote tunahitaji kupanga Mji wetu alisisitiza .
Nae mwenyekiti wa jumuiya ya 
wafanyabiashara Tanzania (JWT) mkoa wa Pwani ,Abdallah Ndauka 
alimshukuru mkuu wa mkoa kwa kutoa muda huo ili kutekelezwa agizo hilo 
na halmashauri.
Ndauka 
alisema kuwa utekelezaji wa ujenzi wa soko hilo umechukua muda mrefu 
kutokana na baadhi ya watendaji kutowajibika ipasavyo na kusababisha 
mipango mingi kushindwa kukamilika.
Awali mkurugenzi wa mji wa Kibaha 
Jeniffer Omolo , alikuwa na wakati mgumu baada ya wafanyabiashara kuinua
 mabango wakitaka mkurugenzi huyo atumbuliwe ama mkuu wa mkoa wa Pwani 
aondoke nae wakidai ameshindwa kuwajibika .
Kufuatia hali hiyo mhandisi Ndikilo ,alisema anatoa muda wa 
miezi mitatu kuitisha mkutano mbele ya wananchi ambao watapiga kura 
endapo kutakuwa na mtendaji ambae ni kero na ataondoka nae.
Alisema serikali
 ya sasa si ya kubembelezana kwani inahitaji watumishi wa umma  
wanaowatumikia wananchi badala ya kufanya kazi kwa mazoea.
Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kibaha Jennifer alieleza  kwamba mchoro wa soko ulizinduliwa tangu mwaka 2014 .
Alisema tatizo kubwa ni uhaba wa fedha licha ya mpango uliopo ni kumaliza ujenzi  mapema iwezekanavyo.
Jennifer alisema  soko kwa sasa litahamia eneo la Sagulasagula na fedha zipo na tangazo la kumpata mkandarasi limeshatoka.
Alisema endapo zoezi la bomoa bomoa 
litafanyika itawasaidia halmashauri kupanga Mji na kuwa na kujenga 
mabanda ya kupumzikia abiria eneo la stend ya sasa.
Kwa mujibu wa Tanroads mkoani 
Pwani,awali zoezi hilo lilikuwa lifanyike mwezi agost lakini muda 
uliongezwa hadi mwezi novemba na kudai wapo watu wengine walishawekewa 
alama ya X tangu mwaka 2004 .
“Sheria
 ya barabara ya mwaka 1932 na kufanyiwa marekebisho 1958 kifunga na 52 
na marekebisho ya sheria ya barabara na 13 ya mwaka 2007 “
Taratibu
 za sheria za usimamizi wa barabara kifunga na 30 (b) eneo la hifadhi ya
 barabara,mita 120 sawa na futi 400 kwenda kila upande kutoka katikati 
ya barabara ni marufuku kufanya maendelezo yoyote katika eneo hilo.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni