Ijumaa, 21 Oktoba 2016

MVUVI AFARIKI AKIVUA BAHARINI MICHEWENI PEMBA


bah
Na Masanja Mabula –Pemba ..
 
MZEE  mmoja anayejulikana kwa jina la Saleh Ali Mbwana mwenye umri wa miaka 45 mkaazi wa Maziwang’ombe Wilaya ya Micheweni  amefariki dunia baada ya kuzama maji   baharini akiwa katika shuhuli zake za  uvuvi .
 
Akidhibitisha kutokea kwa tokeo hilo kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Kamishna Msaidizi Haji Khamis Haji  amesema tukio hilo limetokea oktoba 20  mwaka huu majira ya saa saba za mchana katika bahari ya Maziwang’ombe .
 
Amesema kwamba kabla ya kifo chake , marahemu aliondoka nyumbani kwake kwenda baharini kuvua , na alifikutwa na mauti hayo katika bahari  wakati akitekeleza shuhuli zake za uvuvi.
 
Kkufuatia kutokea kwa tukio hilo Kamanda Haji  amewataka wananchi hususani wanaotoka maeneo ya ukanda wa bahari wanapokwenda kuvua au kulima mwani  kufuatana na wenzao ili patakapo tokea hitilafu waweze kusaidiana .
 
“Wito wangu kwa wananchi ni kuacha kwenda baharini aidha kwa uvuvi au kulima mwani wakiwa mmoja mmoja , bali wafuatane na wenzao ili kuweza kusaidiana panapotokea matatizo ”alisisitiza.
 
 Akizungumza baada ya uchunguzi daktari dhamana wa hospitali ya Wilaya ya Micheweni Dk  Rashid Daudi Mkasha amesema chanzo cha kifo chake kimesababishwa na kukosa hewa  baada ya kukaa nchini ya bahari kwa muda mrefu .
 
Alifahamisha kwamba kitendo cha kukaa chini ya maji  baharini kumesababisha kunywa maji mengi na kupelekea kukosa uwezo wa kuvuta hewa kutokana na maji aliyokunywa bila kutegemea.
 
“Uchunguzi wa kitaalamu umebainisha kwamba kifo kimesababishwa na kunywa maji mengi wakati akiwa chini ya maji ya bahari pamoja na kukosa uwezo wa kuvuta pumzi ”alifahamisha.
 
Mashuda wa tukio hilo  ambao hawakutaka kutajwa majina  yao wameeleza kuwa kabla ya kifo chake Saleh aliondoka nyumbani kwake kuelekea baharini kutafuta riziki na kukutwa na mauti .
Mwili wa marehemu ulikabidhiwa kwa ngudu na jamaa baada ya kufanyiwa uchunguzi na dk wa Serikali ambapo mazishi yake yalifanyika katika maburi ya Maziwang’ombe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni