Brasbend
ya Chipkizi ikiongoza maandamano ya uzinduzi wa mabaraza ya vijana
Jimbo la Magomeni katika shamrashamra za uzinduzi wa mabaraza hayo
uliofanyika uwanja wa Magae Meya Mjini Zanzibar.
Sabra Abdalla Amer akisoma risala ya vijana katika uzinduzi wa mabaraza ya vijana Jimbo la Magomeni.
Mwenyekiti
wa mabaraza ya Vijana Jimbo la Magomeni Kassim Lila Msoma akimkaribisha
mgeni rasmin katika uzinduzi wa mabaraza ya vijana Jimbo la Magomeni,
Mkuu wa Wilaya ya Mjini Bi. Marina Joel Tomas (hayupo pichani).
Mkuu
wa Wilaya ya Mjini Bi. Marina Joel Tomas akizungumza na Vijana wa Jimbo
la Magomeni katika uzinduzi wa mabaraza ya Vijana Jimbo la Magomeni
kabla yakulizindua rasmin Baraza hilo Julay 16, (kulia) Mbunge wa Jimbo
hilo Jamal Kassim Ali na (kushoto) Mwenyekiti wa mabaraza ya Vijana
Jimbo la Magomeni Kassim Lila Msoma.
Baadhi
ya Vijana wa mabaraza ya vijana Jimbo la Magomeni wakimsikiliza Mgeni
rasmin Mkuu wa Wilaya ya Mjini Bi. Marina Joel Tomas hayupo (pichani)
wakati wa uzinduzi huo.
Mkuu
wa Wilaya ya Mjini Bi. Marina Joel Tomas na Mbunge wa Jimbo la Magomeni
Jamal Kassim Ali wakiwapungia mkono Vijana kuwaaga baada ya uzinduzi wa
mabaraza ya Vijana Jimbo la Magomeni.
Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.
………………………………………………………………………………………..
Na Maryam Kidiko/Maelezo Zanzibar.
“Serikali ni muhimu kusimamia
tamaduni na mila za kizanzibar ili sisi vijana tuweze kufata njia
walizopita viongozi wetu na sio kuvuruga mila hizo” Alisema Mwenyekiti
huyo.
Akizitaja changamoto mbali mbali
zinazowakabili katika jimbo lao alisema vijana hawana elimu ya kutosha
ya ujasiriamali hivyo hupelekea vijana wengi kutegemea ajira kutoka
Serikalini jambo ambalo hurejesha nyuma maendeleo ya vijana na
kujiingiza katika utumiaji wa madawa ya kulevya pamoja na uhalifu .
Hata hivyo alisema vijana hawana
ofisi, vianzio vya kuanzishia miradi pamoja na vitendea kazi vitavyoweza
kuwaendeshea miradi mbali mbali katika mabaraza yao.
Uzinduzi wa mabaraza ya vijana umefikia mwisho kwa Wilaya ya Mjini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni