NAIBU WAZIRI AGELINA MABULA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA WIZARA YA ARDHI
By Newsroom May 9, 2016
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula
akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba
na maendeleo ya Makazi uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukubi wa
mikutano wa Shirika la Nyumba Upanga jijini Dar es salaam, Naibu Waziri
Angelina Mabula amewaasa wafanyakazi wa wizara hiyo kufanya kazi kwa
nidhamu na uadilifu kwani kumekuwa na malalamiko kutoka katika
halmashauri mbalimbali nchini wananchi wakilalamikia wafanayakai wa
idara za Ardhi jambo ambalo ziyo zuri, Jirekebisheni mfanye kazi kwa
maslahi ya watanzania ili wananchi waweze kutatuliwa shida zao katika
masuala ya migogoro ya ardhi bila matatizo wala vikwazo.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Bw. Yamungu Kayandabila akimkaribisha Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula
ili kufungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo katika
mkutano uliofanyika mwishoni mwa wiki Upanga jijini Dar es salaam.

Baadhi ya wafanyakazi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula
akiwa ameketi meza kuu pamoja na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Bw. Yamungu
Kayandabila watatu kutoka kushoto pamoja viongozi wa Baraza la
Wafanyakazi Wizara ya Ardhi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni