Alhamisi, 31 Machi 2016

REA KUJA KIVINGINE


 


NA RAYMOND URIO, Dar

WAKALA wa Usambazaji wa Nishati ya Umeme Vijijini (REA), wametoa tamko kuwa kusitisha kwa Bodi ya Shirika la Changamoto (MCC), kutoa misaada nchini haitaathiri mradi wa usambazaji umeme vijijini.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usambazaji wa Nishati ya Umeme vijijini  Letungano Mbakahesya, wakati akitoa tathimini ya maendeleo ya mradi huo ambao kwa mara ya kwanza ulinza kusambaza umeme vijijini mwaka 2007.

Mwakahesya, alisema katika mradi huo serikali inachangia fedha kwa kiasi cha asilimia 90 huku asilimia nyingine ikipatikana kutoka kwa makampuni binafsi.

“MCC haijawahi kutupatia kiasi chochote cha fedha , hivyo , kustisha kutupatia msaada hakutaathiri jambo lolote, usambazaji utaendelea kama ulivyo na huduma itakuwepo katika vijiji vyote tulivyokusudia kutoa huduma hiyo” alisema Mwakahesya

Mkurugenzi mtendaji wa wakala wa Nishati ya umeme vijijini. Lutengano Mwakahesya, akizungumza na waandishi wa habari jana, jijini, Dar es Salaam kuhusiana na jinsi umeme huo ulivyosambazwa kwa maeneo ya vijini. Kushoto Meneja wa wakala wa Nishati ya umeme vijijini Elineema Mkumbo.

Alisema lengo la mradi huo ni kusanbaza umeme katika vijiji 15,000 nchini hadi kufikia sasa wameshasambaza umeme katika vijiji 520 ambayo sawa na asilimia 36 huku wakifikia idadi ya watumiaji 75,000 ikiwa matarajio yao kufikia watumiaji 250,000.

Alisema kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa mradi huo walianza na Sh. Bilioni 10 na kufanikiwa kusambaza umeme katika Wilaya za vijiji vitano ambavyo ni Kilolo, Mkinga, Kilindi, Uyuhi na Bahi.

 

“Baada ya kusambaza katika vijiji hivyo tuliona mafanikio, serikali kwa mara ya kwanza ilitupatia Sh. bilioni 120 ambapo mchango mwingine ulitoka shirika la usambazaji umeme Tanzania (Tanesco), na kusaidia fedha hizo kusambaza mradi katika vijiji saba na maeneo mengie ya biashara ’’ alisema.

Mwakahesya, alisema utekelezaji wa awamu ya pili  ulianza mwaka 2013 hadi 2016 walipatiwa Sh. bilioni 881 ya usambazaji wa umeme huo  vijijini na kufikia asilimia 90 ya utekelezaji  na kutegemea ifikapo mwezi Juni mwaka huu utekelezaji utakuwa umekamilika katika vijiji vyote walivyovikusudia hapa nchini.

Alisema baada ya mradi wa awamu ya pili kukamilika imetengwa Sh. bilioni 584 kwa mwaka wa fedha 2016- 2017 kwajili ya awamu ya tatu ambayo itaendelea kusambaza umeme katika vijiji vingine ambavyo awajafikiwa na mladi huo kwa awamu nyingine zilizopita hapo awali.

Meneja wa Usambazaji wa umeme huo Elineema Mkumbo, aliyataja mashirika binafsi ambayo yanawasaidia kusambaza umeme kutokana na Tanesco kwa sasa awawezi kufika vijijini huko ambayo ni shirika la Lifti Vale ambalo linaunganisha umeme kutoka Mufindi na kuusambaza katika vijiji 14 na kiasi kinachobaki kukiunganisha katika gridi ya taifa.

“Tasisi nyingine tunazoshirikiana nazo ni Lumama ipo Wilaya ya Ludewa inazalisha umeme na kusambaza katika vijiji 6, tasisi nyingine ipo mkoani Ruvuma inaitwa Chipole inazalisha megawati 5 na kusambaza umeme Songea na kusaidia matumizi ya mafuta ya disel kupungua, tasisi nyingine Ndoa ambayo inasambaza umeme nusu megawaiti  katika kijiji cha Mbinga ’’.

Alisema wawekezaji wanaohitaji kuwekeza katika mradi huo wanakaribisha na watanzania wategemee huduma bora ya umeme pindi mladi huo utakapokamilika  katika maeneo hayo ya vijjini.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni