Jumatano, 11 Mei 2016

 

RAIS MSTAAFU DK. JAKAYA KIKWETE AHANI MSIBA WA MAMA YAKE NA TEDDY MAPUNDA

JY01 
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk Jakaya Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakisalimiana na Teddy Mapunda pamoja na Ndugu na Jamaa wa familia wakati alipofika Mbezi nyumbani kwa wafiwa kwa ajili ya kuhani msiba wa mama mzazi wa Teddy Mapunda Marehemu Benadette Izengo ambaye alizikwa juzi katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
JY1 
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk Jakaya Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakisaini kitabu cha Maombolezo mara baada ya kuwasili Mbezi nyumbani kwa Teddy Mapunda kwa ajili ya kuhani msiba huo.
JY2 
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha Maombolezo huku Mama Salma Kikwete akiwa amesimama nyuma kulia ni Teddy Mapunda Mtoto wa Marehemu Benadette Izengo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni