BAADA YA KADI NYEKUNDU IBRAHIM AJIB ATIMKIA ZAKE SAUZ....
Mshambuliaji Ibrahim Ajib wa Simba ametimkia nchini Afrika Kusini.
Taarifa zinaeleza, Ajib anakwenda kufanya majaribio katika timu ya Kaizer Chiefs lakini uongozi wa Simba, haukuridhia.
Kutoka
ndani ya Simba, taarifa zinaeleza Ajib aliomba ruhusa kwenda Afrika
Kusini kupitia mtu aitwaye Ndambile mara baada ya mechi dhidi ya Mwadui
FC.
“Sasa hiyo ikashangaza sana, kweli mtu anakwenda majaribio anaweza kuomba ruhusa saa chache kabla ya kuondoka.
“Kwani majaribio ni suala la kushitukiza, hakika imewashangaza sana viongozi na hawakutoa ruhusa lakini ameondoka.
“Hii
inaanza sasa kuhusisha na ile kadi nyekundu aliyepata katika mechi
dhidi ya Mwadui. Maana haikuwa na sababu, sasa alifanyaje hivyo, au
ndiyo alitaka apate nafasi ya kwenda Afrika Kusini?” kilieleza chanzo.
Ajib
ni kati ya wachezaji waliokulia Simba kisoka na amepata mafanikio
mwanzoni au katikati ya msimu. Lakini mwishoni ameonekana kupungua
makali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni