Alhamisi, 31 Machi 2016

Yondani aibuka shujaa wa Mechi



NA RAYMOND URIO, Dar



Mchezaji wa Yanga Fc, Juma Abdul Abdul akithibitiwa na beki wa Ndanda Fc

KlABU ya Yanga imetinga nusu fainali katika Kombe la Shirikisho FA maarufu baada ya kuilaza 2-1 Ndanda FC ya Mtwara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga walitangulia kupata bao lao dakika ya 27 kupitia kwa mshambuliaji wake, Paul Nonga aliyeunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu uliopigwa na beki wa kulia Juma Abdul.
Adhabu hiyo ilitolewa baada ya kiungo na Nahodha wa Ndanda, Kiggi Makassy kumchezea faulo mshambuliaji wa Yanga, Mzimbabwe Donald Ngoma nje kidogo ya boksi.
Katika kipindi hicho, Yanga wangeweza kuondoka na mabao zaidi kama washambuliaji wake, wangekuwa makini hususan Nonga mwenyewe na mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu uliopita, Simon Msuva.
Msuva alipewa pasi nzuri kwenye njia na Kamusoko dakika ya 34, lakini akagongesha mwamba wa juu, wakati Nonga naye alipewa pasi nzuri na Mzimbabwe huyo na wakati anajivuta kupiga shuti ndani ya boksi beki wa Ndanda, Paul Ngalema akaupitia mpira na kuondosha kwenye hatari.
Kipindi cha pili, Ndanda walifanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 56 kupitia kwa Nahodha wake, Kiggi Makassy kwa shuti la nje ya boksi baada ya kuwatoka mabeki wa Yanga.
Baada ya bao hilo, Yanga walicharuka na kufanikiwa kupata bao la ushindi lililofungwa na beki Kevin Patrick Yondan kwa penalti dakika ya 69, baada ya beki wa Ndanda, Paul Ngalema kumkwatua winga Simon Msuva ndani ya boksi.

Azam Fc Yatinga nusu fainali FA



 
Wachezaji wa Azam Fc wakishangilia ushindi .
NA RAYMOND URIO
KLABU ya Azam FC imetinga nusu fainali ya Kombe la Shirikisho FA kwa kuichapa Prisons kwa mabao 3-1.

Kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam, timu hizo zilionyesha upinzani mkubwa katika kipindi cha kwanza.

Ulikuwa ni upinzani mkali kati ya timu hizo mbili lakini Azam FC ndiyo waliokuwa makini kuzitumia nafasi walizozipata kupitia mchezaji wao na beki wa timu hiyo Shomari Kapombe aliyefunga mabao mawili na Hamis Mcha aliyefunga bao moja.

Jeremiah Juma ndiye alifunga bao pekee la Prisons ambayo kila muda ulivyokuwa ukisonga mbele ilionekana kupoteza kasi na umakini.


Azam FC inakuwa ni timu ya tatu kutinga nusu fainali ya Kombe la FA baada ya Mwadui FC na Yanga.

EBOUE HATIANI KLABUNI SUNDERLAND



KLABU ya Sunderland imemfukuza beki wake Emmanuel Eboue baada ya 22  kufuatia taarifa za kufungiwa mwaka mmoja kwa kushindwa kumlipa wakala wake wa zamani.
Mapema asubuhi ya leo (jana), Shirikisho la Soka Duniani, FIFA imesema leo nyota huyo wa zamani wa Arsenal mwenye umri wa miaka 32 hataruhisiwa kujishughulisha na soka hadi atakapomlipa wakala wake Sebastien Boisseau, anayemdai kiasi cha Pauni Milioni 1.
Sunderland imechukua hatua za haraka kwa kumvunjia Mkataba mchezaji huyo  licha ya kwamba alikuwa hajaripoti kuanza kazi kwenye klabu hiyo baada ya kujiunga nayo kama mchezaji huru Machi 9.
  Eboue akiwa ameshika jezi ya Sunderland baada ya kusajiliwa.
Emmanuel Eboue amefungiwa mwaka mmoja na FIFA hadi hapo atakapomlipa wakala wake wa zam

Pamoja na hayo, Eboue anaweza kurejeshwa kikosini Sunderland iwapo atamalizana na wakala wake kwa kulipa deni hilo ndani ya wiki mbili zijazo.

AL AHLY YAIPA UBINGWA YANGA




 NA RAYMOND URIO
Klabu ya Al Ahly ya Sudan haitakuja tena nchini Tanzania jijini, Mwanza kumenyana na Yanga katika Kombe la Shrikisho la Soka Afrika (CAF), baada ya kuandika barua FIFA ikisema inakabiliwa na hali mbaya kiuchumi.
Maana yake Yanga wanasonga mbele bila jasho baada ya wapinzani wao hao kujitoa na sasa watamenyana na mshindi kati ya Azam FC ya Msumbiji na USM Alger ya Afrika Kusini.








KIKOSI CHA AL AHLY,( LEO NI SIKUKUU YA WAJINGA GOOD DAY                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                          

MOI YAPOKEA MILIONI 20



TAASISI YA TIBA YA MIFUPA, UPASUAJI WA UBONGO NA MISHIPA YA FAHAMU (MOI) YAPOKEA MILIONI 20

  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa ,Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) Dk. Othman Kiloloma akizungumza wakati alipokua akipokea msaada kutoka, Taasisi ya GSM ya Dar es Salaam baada ya kumkabidhi hundi ya mfano ya Milioni 20 kwa ajili ya kununulia vifaa tiba na matibabu kwa watoto wenye matatizo ya vichwa vikubwa na mgongo wazi ambao unajulikana kama Hydrocephalus & Spinal Bifida. Jijini, Dar es Salaam leo (PICHA NA RAYMOND URIO)

NA MWANDISHI WETU

Taasisi ya GSM ya Dar es Salaam, imekabidhi msaada wa fedha taslimu shilingi milioni 20, kwa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) kwa ajili ya kununulia vifaa tiba na matibabu kwa watoto wenye matatizo ya vichwa vikubwa na mgongo wazi ambao unajulikana kama Hydrocephalus & Spinal Bifida.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mfano wa hundi, mwakilishi wa Kampuni ya GSM, Shannon Kiwamba, alisema wameguswa na changamoto zinazowakabili Watanzania ndiyo maana imeamua kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Dkt John Pombe Magufuli ya kuboresha huduma za afya hapa nchini.

Shannon alisema, pamoja na msaada wa fedha ambazo GSM imeipa Moi, vilevile watafadhili kambi za upasuaji (Surgical camps) kwa watoto wenye matatizo ya vichwa kujaa maji na mgongo wazi katika mikoa mitano ya Kanda ya Ziwa.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Moi, Dkt Othman Kiloloma, alisema anaishukuru GSM kwa kuguswa na hali za Watanzania hususan watoto wenye matatizo ya vichwa kujaa maji na mgongo wazi ambao kimsingi wanahitaji kufarijiwa.

Dkt kiloloma aliongeza, GSM imefanya uamuzi sahihi wa kuunga mkono jitihada za Serikali kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya kwa wakati mwafaka.
Alisema, fedha zilizotolewa na GSM zitatumika kama ilivyoelekezwa, vilevile Moi ipo tayari kutoa wataalamu kwenda mikoani kuwafanyia upasuaji watoto katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ili kuwapunguzia wagonjwa adha ya kusafiri kwenda Dar es Salaam.

Taasisi ya Moi imekuwa ikichukuwa jitihada madhubuti za kuhakikisha Watanzania hususan watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi wanapata huduma bora pale walipo, ambapo imekuwa ikipeleka wataalam mikoani kwa ufadhili wa wadau mbalimbali na kuwafanyia upasuaji.

Takwimu zinaonesha hapa Tanzania watoto zaidi ya 5,000 kwa mwaka wanazaliwa na vichwa vikubwa na mgongo wazi ambapo watoto 400 mpaka 500 pekee ndiyo wanapokelewa Moi.