Pombe za asili zatamba soko la vinywaji nchini
Wafanyakazi wa DarBrew wakionyesha kinywaji cha Chibuku kwenye chupa ndogo wakati wa kuizindua hivi karibuni

Kikosi
kazi cha menejimenti na wafanyakazi wa DarBrew wakiwa katika picha ya
pamoja wakati wa kusherehekea kupata tuzo ya SABMiller ya kuendeleza
vinywaji vya asili nchini hivi karibuni.
…………………………………………………………………………………………………………..
-TBL Group yajipanga kuziboresha kulinda afya za watumiaji na kuchangia pato la Taifa
Licha ya
kuwepo na viwanda mbalimbali vya kutengeneza bia na vinywaji vingine vya
kisasa ikiwemo uingizwaji wa vinywaji hivyo kutoka nje ya nchi bado
idadi kubwa ya watanzania wanatumia pombe za asili na sababu kubwa
inabainishwa kuwa hali hiyo inatokana na vinywaji vya kisasa kuuzwa kwa
bei ya juu.
Utafiti
uliofanywa na taasisi ya CanBack kuhusiana na matumizi ya pombe za
asili nchini umebainisha kuwa matumizi ya pombe za asili nchini ni
asilimia 50% ambapo kati ya asilimia hizo vinywaji vya asili
vinavyototengenezwa kisasa viwandani vinatawala kwa asilimia 8% .
Sababu kubwa
ya watumiaji wa vinywaji vya asili ambavyo vingi vinatengenezwa kwenye
mazingira yasiyo salama na vinaendelea kuleta athari kwenye jamii ni
kutokana na bei kubwa ya bia ,wine na vinywaji vinginevyo vya kisasa
ambapo idadi kubwa ya wananchi hawana uwezo wa kumudu kuvinunua na
kuvitumia.
Akitoa
ripoti ya utendaji wa kampuni katika kipindi cha mwaka 2015 na mikakati
yake ya mbele katika kipindi cha mwaka 2016/17 kwa waandishi wa habari
hivi karibuni,Mkurugenzi Mkuu wa TBL Group,Roberto Jarrin alisema kuwa
kampuni yake tayari imeanza kutekeleza mkakati wa kuboresha vinywaji
vya asili na kuhakikisha vinaingia katika mfumo rasmi unaotambulika kwa
kuviwezesha kuchangia pato la taifa kwa njia ya kodi ikiwemo kulinda
afya za wananchi.
Jarrin
alibainisha kuwa kampuni ya DarBrew imeweza kuleta mapinduzi ya uuzaji
wa pombe za asili nchini kwa kuwawezesha watumiaji kupata kinywaji cha
Chibuku na Nzagamba kikiwa kimefungwa kwa viwango mbalimbali na katika
mazingira ya usafi yanayolinda afya za watumiaji na hivi sasa imekuja na
mkakati wa kuwainua akina mama kimapato kupitia kuuza bidhaa zake
unaojulikana kama Chibuku Mamas ambao hadi kufikia sasa wanawake wapatao
130 wameishajiunga na mpango huu.
Alisema kuwa
akina mama wakiendelea kujiunga na mpango huu wataweza kujikwamua
kimapato na kulinda afya zao na wanywaji pia kupunguza uharibifu wa
mazingira kwa kutumia kuni kwa ajili ya kupikia pombe za asili ambazo
zimekuwa zikiuzwa katika vilabu mbalimbali.”Tunawasihi watumiaji wa
vinywaji vya asili kujenga mazoea ya kutumia vinywaji vyenye ubora na
vilivyotengenezwa kwenye mazingira mazuri kwa ajili ya kulinda afya zao”.Alisema
Katika
kuhakikisha watumiaji wanamudu vinywaji vya asili vya Chibuku na
Nzagamba alisema kampuni imeanza kusambaza vinywaji hivi vikiwa kwenye
ujazo wa chupa za ukubwa wa aina mbalimbali ili wanywaji wote waweze
kuvipata kulingana na vipato vyao.
Kuhusu
mtazamo wake wa hali ya biashara ya kampuni kwa sasa Jarrin alisema
sekta ya uuzaji wa vinywaji inakabiliwa na changamoto mbalimbali
mojawapo ni bei kubwa ya bia ambayo watumiaji wake wengi wanashindwa
kuimudu,kuwepo na vinywaji visivyo katika mfumo rasmi wa ushindani
katika soko,kukosekana kwa motisha katika uzalishaji wa malighafi za
kutengeneza vinywaji nchini kwa kuwa zinatozwa kodi kubwa ya zuio kuliko
malighafi zinazotolewa nje ya nchi.
Alisema
baadhi ya mambo yanayostahili kufanyika katika uboreshaji wa sekta ili
iendelee kuchangia pato la taifa ni kupunguza kodi za malighafi
zinazozalishwa nchini kama kimea kinachotumika kutengeneza bia pia
kulasimisha pombe za asili ziende sambamba na vinywaji vya sili
vinavyolipiwa kodi na kuhakikisha vinywaji vya asili vinapatikana
katika mazingira ya usafi “Pamoja na changamoto nyingi zilizopo
katika sekta hii tunaendelea kukabiliana nazo na tumedhihirisha uwezo
wetu kwa kuwa na viwanda vyenye ubora wa hali ya juu nchini
Tanzania”Alisema Jarrin
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni