MBUNGE WA JIMBON LA KIKWAJUNI MHANDISI HAMAD MASAUNIN AKABIDHI JEZI ZA MASHINDANO

Mbunge
wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimkabidhi nahodha wa
timu ya Mkunazini, Ahmed Omari Haji , jezi zitakazotumiwa na timu yake
wakati wa Kombe la Masauni -Jazeera, linaloanza kutimua vumbi leo katika
Viwanja vya Mnazi Mmoja,Zanzibar. Wapili kulia ni Diwani wa kata ya
Miembeni, Mbaruku Abdallah Hanga.
Nahodha
wa timu ya Kikwajuni Bondeni, Salum Said (kushoto), akipokea jezi
kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia).

Mbunge
wa Jimbo la Kikwajuni, ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watatu kushoto), akiwa na baadhi
ya viongozi na makocha wa timu zinazotarajiwa kuanza kumenyana katika
mashindano ya Kombe la Masauni-Jazeera, muda mfupi baada ya kukagua
Uwanja wa Mnazi Mmoja utakaotumika kwa mashindano hayo.(Picha na Mpiga Picha Wetu)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni