Alhamisi, 12 Mei 2016

NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI FROF. JAMES MDOE AFUNGA MKUTANO WA JOTOARDHI JIJINI DAR ES SALAAM

ta1 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  madini, Prof. James Mdoe ( wa nne kutoka kulia) akisoma hotuba ya ufungaji wa mkutano wa siku tatu uliokutanisha wataalam wa  masuala  ya jotoardhi kutoka katika nchi  za Tanzania,  Kenya,  Uganda, Rwanda, Ethiopia, Eritrea, Marekani, New Zealand na Djibouti kwa ajili ya kujadili  taarifa ya mtaalam mwelekezi  kuhusu utafiti uliofanywa katika Ziwa Ngozi lililopo mkoani Mbeya ambapo kuna  viashiria  vya  jotoardhi pamoja na eneo la  Kibiro nchini Uganda.
ta2 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  madini, Prof. James Mdoe (kushoto) akisisitiza jambo wakati alipokuwa akifunga mkutano huo. Kulia ni Mjiolojia Mkuu kutoka Idara ya Nishati, Wizara ya Nishati na Madini, Jacob Mayalla.
ta3 
Sehemu ya washiriki wa mkutano huo wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufungaji iliyokuwa inatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  madini, Prof. James Mdoe (hayupo pichani)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni