NA RAYMOND URIO, Dar
KATIKA
kuhakikisha sekta kilimo na wafanyabishara na watu waliochini ki maisha hapa nchini Shirika lisilo lakiserikali la
Mastercard Fundation For Rural prosperity, limeanzisha miradi ya mikopo katika kuwasaidia
wakulima wadogo na wafanyabiashara, watu walio katika hali ya chini ili kuwawezesha kiuchumi na kuondokana na hali ya umasikini.
Mikopo yenye
thamani ya dola za kimarekani milioni 35 fedha hizo zitagawiwa katika vikundi
vya akiba,bima na mikopo kwa manufaa ya karibu takribani milioni 8, katika maeneo ya vijijini kwa Afrika vinavyojishughulisha na kilimo, wafanyabiashara na walipo katika kaya masikini zilizopo
vijijini katika nchi za bara la Afrika.
Baadhi ya Wadau wakimsikiliza Mtaalam, Mshauri wa Kiufundi wa Shirika hilo kwenye mkutano huo leo Maelezo jijini Dar es Salaam. Picha na Raymond Urio
Akizungumza
na waandishi wa habari Mshauri wa taasisi hiyo Gabriel Kivuti amesema kuwa
kwakushirikiana na taasisi zakifedha zilizopo hapa nchini taasisi hiyo imeamua
kutoa fedha ambazo sio za mkopo ilikuweza kumsaidia kiuchumi wakulima
na wafanya biashara wadogodogo.
‘’Katika
kipindi cha mwaka jana taasisi yetu imetoa zaidi ya dola zakimarekani milioni 35
ikiwa nalengo lakuwasaidia wakulima wadogo wawadogo mradi huu wa mfuko kwa ajili
yamaendeleo vijijini unasimamiwa na Taasisi ya KPMG international Development
advisor services Afrika ‘’Alisema Mshauri Gabriel KIVUTI .
Mshauri
Kivuti alisema kuwa kumekuwepo na changamoto nyingi katika kaya nyingi zilizopo
vijijini barani afrika kutoshirikishwa katika masuala yakifedha ambapo zaidi ya
asilimia 70 kaya masikini zilizokusini
mwajangwa la sahara zimekuwa zikitegemea kilimo kama uti wa mgongo wauchumi .
Mtaalama Mshauri wa Kiufundi wa Shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na maendeleo ya vijijini lijulikanalo kama MasterCard Foundation, for Rular Prosperity, Gabriel Kivuti akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na kuwatangaza washindi wa tuzo kwa makampuni matano yenye thamani ya Dola za Kimarekani 10 kwaajili ya kukuza uchumi wao. Picha na Raymond urio
Alisema
wakulima wadogo wadogo wamekuwa wakikabiliwa nachangamoto ya baadhi ya taasisi
za kifedha kuweza kuwafikia katika maeneo yao hali inayozorotesha jitihada za
kukwamua sekta ya kilimo na wakulima wenyewe.
‘’Gharama
kubwa zakufanya biashara ,ukosefu wa wafanyakazi wenye ujuzi namiundo mbinu
yabiashara isiyo badilika inazorotesha jitihada za kupanua bidhaa sahihi ambazo
zingeweza kuwasaidia kaya masikini’’Aliongeza KIVUTI.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni