PROF. MAKAME MBARAWA AZINDUA BODI YA TPA

Wajumbe
wa Bodi mpya ya Bandari Nchini (TPA), wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, wakati wa uzinduzi wa
bodi hiyo.

Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akitoa
maelekezo kwa Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Hebel Mhanga
alipokagua eneo la kupakulia makontena bandarini hapo.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Nchini (TPA), Eng.
Aloyce Matei (wa kwanza kushoto), akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kushoto),
alipokagua miundombinu ya Bandari ya Dar es Salaam.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akitoa
maelekezo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari
Tanzania (TPA), Profesa Ignas Rubaratuka (kushoto), wakati alipokagua
eneo la kuhifadhia magari katika bandari ya Dar es Salaam.
Habari Picha na Benjamini Sawe-Maelezo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni