Jumatano, 26 Julai 2017

NA RAYMOND URIO

MBUNGE wa Jimbo la Manonga kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Seif Khamis Gulumali amefanya ziara katika kata ya Ntobo Kaskazini, Ngulu, Mwashiku na Choma kwenye Wilaya ya Manonga jana ikiwa ni sehemu ya kutekeleza ilani ya Chama hicho.
   

     Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akizungumza na wananchi wa kata ya Ntobe kaskazini iliyoko katika Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora katika moja ya ziara yake leo. wa pili kulia ni Diwani wa kata hiyo, Emmanuel Samson. (Picha zote na Raymond Urio)

Awali Mbunge Gulamali aliwasili katika kata ya Ntobo Kaskazini na kujionea maendeleo yanayoendelea kwenye kata hiyo na kuhaidi kuendelea kutoa huduma kadiri inavyowezekana. Hata hivyo Mbunge Gulumali alitoa shukrani kwa wanachi wote walio weza kumchagua ili kuwa mbunge wao na kuweza kuwatumikia.

'Na washukuru wananchi wote wa Kata ya Ntobo kwa kuweza kunichagua na kuwa kiongozi wenu hivyo wajibu wangu ni kuendelea kuwahudumia kama niliweza kuhaidi. alisema Gulumali.
Hata hivyo Gulamali amechangia mabati 20 pamoja na mbao 50 za ujenzi wa ofisi za Chama hicho katika Kata hiyo. Lakini pia Diwani wa kata hiyo Emmanuel Samson alitoa shukrani kama sehemu ya kuwawakilisha waanachi wa kata hiyo kwa msaada huo pamoja na kuhaidi kumuunga mkono Mbunge huyo.

        Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akisikiliza maoni ya wananchi wa kata ya Ntobe kaskazini iliyoko katika Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora katika moja ya ziara yake leo. kulia kwake ni Diwani wa kata hiyo, Emmanuel Samson.

Hata hivyo Mbunge Gulamali aliweza pia kuwatembelea wanachi wa kata ya Ngulu, kwa kuangalia maendeeo yanayoendelea baada ya awali kuchangia fedha kwaajili ya ukarabati wa barabara ya barabara kwenye kata hiyo.

Lakini pia Gulamali amehaidi kuchangia mifuko ya seruji kwa ajili ya kutengeneza choo cha Hospitali na nyumba ya Mganga Mkuu katika Hosptali ya kata.

     Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akisikiliza maoni ya wananchi wa kata ya Mwashiku iliyoko katika Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora katika moja ya ziara yake leo.


Hata hivyo Gulamali aliweza pia kutembelea wananchi wa kata ya Choma pamoja na Mwashiku na kuwaeleza juu ya ufufuaji wa kiwanda cha ... kilichokuwa kimetelekezwa na Mmilimki .... wa kiwanda hicho kwamuda mrefu bila hata kufanya kazi.



     Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akizungumza na wananchi wa kata ya Choma iliyoko katika Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora katika moja ya ziara yake leo

Lakini pia aliwahaidi pindi kiwanda hicho kitakapo fufuliwa itakuwa ni nafasi nzuri kwa wananchi wa Choma pamoja na wengine walio katika Wilaya ya Igunga ili waweze kupata kazi katika kiwanda hicho na kuweza kuendesha maisha yao na familia zao.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni