Jumamosi, 29 Julai 2017

MBUNGE GULAMALI AFANYA ZIARA YA KUONA MAENDELEO YA UFUFUAJI WA KIWANDA CHA MANONGA GENERY

NA RAYMOND URIO

Mbunge wa Jimbo la Manonga kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Seif Khamis Gulamali leo ametembelea kiwanda cha Manonga Ginery kinachohusika na kutengeneza pamba, kilichokuwa kimesimama kwa takribani miaka ishirini (20) bila ya kufanya.




Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akisaliamiana kwa furaha na mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan leo alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho kilichopo Wilayani Igunga kata Choma. ( Picha zote na Raymond Urio )


Mapema leo hii Mbunge Gulamali aliwasili katika eneo la kiwanda hicho, iliyopo Jimbo la Igunga Kata ya Choma akiwa pamoja na Mmiliki wa kiwanda hicho, ndugu Urvesh Rajan pamoja na viongozi wa Serikali za mitaa, wahandisi na mafundi wa viwanda.

Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (kushoto )akioneshwa moja kamba na mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan zinatokana na zao la pamba katika kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho leo Wilayani Igunga kata ya Choma. Katikati ni katibu wa kiwanda cha Nyuzi Tabora. ( Picha zote na Raymond Urio )
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea na kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho ili kianze kufanya kazi upya, baada ya kukaa kwa miaka kadhaa bila ya kufanya kazi, Mbunge Gulamali alisema, leo nimekuja kuoana maendeleo ya kufufuliwa wa kiwanda hichi ikiwa ni sehemu ya kutaka kutimiza tena ahadi yangu niliyo itoa kwa wanachi wa Igunga na Manonga kwamba lazima kiwanda cha Manonga Ginery, kianze kazi ili wananchi waweze kunufaika katika zao biashara ya pamba na wengine kupata ajira kwa kuendesha maisha na kukuza uchumi wa viwanda nchini.
     
Mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan akizugumza na Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (katikati), alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho leo Wilayani Igunga kata ya Choma. Kushoto ni Mwenyekiti wa Igombensabo Lazaro Ngullo.      
" Leo nimekuja kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hichi ikiwa ni sehemu yangu ya ahadi niliyo itoa kwa wananchi wangu wa jimbo la Manonga pamoja na Igunga kwamba lazima kiwanda hiki kifanye kazi tena, ili biashara ya zao la pamba lirudi tena na wananchi na waweze kupata ajira katika kiwanda hichi pia kukuza uchumi wa nchi ya Viwanda.

" Kufufuliwa kwa kiwanda hiki ni fursa kubwa ya maendeleo kwa jamii ya wana Igunga na Manonga na hasa wakulima wa zao la pamba hata kwa wananchi wanao lilia ajira, hivyo fursa kwa sasa iko wazi, alisema Gulamali.


Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akipewa moja ya maelezo ya mashine ya ya zao la pamba ndani ya kiwanda cha Manonga Genery, leo alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho kilichopo Wilayani Igunga kata Choma.
Hata hivyo Mbunge Gulamali alisema kuwa bila kumpa ujumbe mmiliki wa kiwanda hiki na kutompa matakwa ya wananchi basi ingekuwa sicho kilichotokea leo, kwahiyo nimetumia uongozi wangu kwaajili ya wananchi wangu ili kuona maendeleo yakiendelea tena katika swala kiwanda na kuona zao la pamba likirudi tenaa kwa kasi katika Jimbo la Igunga na Manonga.
    

Mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan akimpa maelekezo Mbunge wa Manonga Seif Khamis Gulamali ndani ya kiwanda hicho (katikati), leo alipotembelea na kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda kilichopo Wilaya ya Igunga kata ya Choma.

Lakini pia Mbunge Gulamali amewataka wakulima wa zao la pamba kuanza kulima kwa kasi kilimo cha hicho kwa kuwa sasa kiwanda hiki kitaanza kufanya kazi, hivyo juhudi na jitihada zenu ndio itakayoweza kufanya kiwanda hiki kiendelee kwa kuwa nao wanategemea pamba toka kwenu na wao waweze kuuza kwa wafanya biashara wakubwa wa nje ya mipaka na ndani ya nchi.

      
Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (kushoto) akizungumza na Mwenyekiti wa Igombensabo, Ndug, Emmanuel Ngullu.
Hata hivyo Mmiliki wa kiwanda hicho, ndug, Urvesh Rajan amemshukuru Mbunge Gulamali sambamba na uongozi wa serikali wa kata ya Choma kwa kuweza kuvumilia kwa kipindi chote tangia kiwanda kilivyo simama na hata pale alitoa ombi lake la kukufua tena kiwanda waliweza kumsikilliza na hivyo ni jambo la kushukuru.

Lakini pia mmiliki wa kiwanda hicho ndug, Rajan ametoa ombi kwa wakulima wa zao la pamba kuweza kujitaidi kulima zao hili kwa kasi, kwa kuwa kiwanda kinategmea sana zao hili na si zao jingine, hivyo pesa watakayo ilipa toka kwawakulima wana imani nao itarudi pale watakapo wauzia wafanya biashara na ndio kiwanda kitazidi kuendelea.


Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akiongozana na viongozi wa serikali pamoja na wahandisi alipotembelea kiwanda hicho leo kilichopo Wilayani Igunga kata ya Choma.

" Ninafurahi Mbunge Gulamali ameitikia wito wangu kwa kuja na kuona maendeleo ya kutaka kufufua kiwanda hichi hivyo, ni jambo zuri kuona kiongozi akiwa sambamba na wewe na mwenye kutaka maendeleo,

" haitochukua muda tutaaenda kuanza kazi hivyo nina waomba wakulima wa zao hili kuchangamkia fursa kwenye ulimaji kwa kuwa fedha watapata za kuendesha maisha hata ajira pamoja na kukuza uchumi wa nchi yetu, alisema. Rajan.

Hata hivyo Mwenyekiti wa kijiji cha Choma, Ndug, Emmanuel Methew alisema kuwa kitendo kilichofanyika leo cha mbunge kuja kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hiki ni kitu kizuri kutokana ni mikaa mingi kutofanya kazi hivyo wakulima walikuwa wanapata tabu katika zao hili, hata mwishowe kukata tamaa katika kulima zao hili kutokana na kufa kwa kiwanda hiki.



Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (katikati) akisikiliza kwa makini maelekezo kutoka kwa mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan leo alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho kilichopo Wilayani Igunga kata Choma.

"Kiwanda kufufuliwa tena ni jambo zuri hivyo nina imani kuwa wakulima watarudisha nguvu zao kwa kasi kwenye zao hili la pamba kwakuwa ndio moja ya zao kubwa katika mkoa wa Tabora, alisema Methew.

Jumatano, 26 Julai 2017

NA RAYMOND URIO

MBUNGE wa Jimbo la Manonga kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Seif Khamis Gulumali amefanya ziara katika kata ya Ntobo Kaskazini, Ngulu, Mwashiku na Choma kwenye Wilaya ya Manonga jana ikiwa ni sehemu ya kutekeleza ilani ya Chama hicho.
   

     Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akizungumza na wananchi wa kata ya Ntobe kaskazini iliyoko katika Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora katika moja ya ziara yake leo. wa pili kulia ni Diwani wa kata hiyo, Emmanuel Samson. (Picha zote na Raymond Urio)

Awali Mbunge Gulamali aliwasili katika kata ya Ntobo Kaskazini na kujionea maendeleo yanayoendelea kwenye kata hiyo na kuhaidi kuendelea kutoa huduma kadiri inavyowezekana. Hata hivyo Mbunge Gulumali alitoa shukrani kwa wanachi wote walio weza kumchagua ili kuwa mbunge wao na kuweza kuwatumikia.

'Na washukuru wananchi wote wa Kata ya Ntobo kwa kuweza kunichagua na kuwa kiongozi wenu hivyo wajibu wangu ni kuendelea kuwahudumia kama niliweza kuhaidi. alisema Gulumali.
Hata hivyo Gulamali amechangia mabati 20 pamoja na mbao 50 za ujenzi wa ofisi za Chama hicho katika Kata hiyo. Lakini pia Diwani wa kata hiyo Emmanuel Samson alitoa shukrani kama sehemu ya kuwawakilisha waanachi wa kata hiyo kwa msaada huo pamoja na kuhaidi kumuunga mkono Mbunge huyo.

        Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akisikiliza maoni ya wananchi wa kata ya Ntobe kaskazini iliyoko katika Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora katika moja ya ziara yake leo. kulia kwake ni Diwani wa kata hiyo, Emmanuel Samson.

Hata hivyo Mbunge Gulamali aliweza pia kuwatembelea wanachi wa kata ya Ngulu, kwa kuangalia maendeeo yanayoendelea baada ya awali kuchangia fedha kwaajili ya ukarabati wa barabara ya barabara kwenye kata hiyo.

Lakini pia Gulamali amehaidi kuchangia mifuko ya seruji kwa ajili ya kutengeneza choo cha Hospitali na nyumba ya Mganga Mkuu katika Hosptali ya kata.

     Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akisikiliza maoni ya wananchi wa kata ya Mwashiku iliyoko katika Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora katika moja ya ziara yake leo.


Hata hivyo Gulamali aliweza pia kutembelea wananchi wa kata ya Choma pamoja na Mwashiku na kuwaeleza juu ya ufufuaji wa kiwanda cha ... kilichokuwa kimetelekezwa na Mmilimki .... wa kiwanda hicho kwamuda mrefu bila hata kufanya kazi.



     Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akizungumza na wananchi wa kata ya Choma iliyoko katika Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora katika moja ya ziara yake leo

Lakini pia aliwahaidi pindi kiwanda hicho kitakapo fufuliwa itakuwa ni nafasi nzuri kwa wananchi wa Choma pamoja na wengine walio katika Wilaya ya Igunga ili waweze kupata kazi katika kiwanda hicho na kuweza kuendesha maisha yao na familia zao.